STEVE NYERERE AFUNGUKA MAZITO KUHUSU BIFU LAKE NA KOLETA

MWENYEKITI wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amefungukia madai ya kumtenga msanii mwenzao, Coletha Raymond ‘Koleta’ kipindi alipokuwa anaumwa.
Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ (mwenye suti).
Awali, madai yalipenyezwa kuwa, klabu hiyo ilimtenga Koleta kipindi alipokuwa akiumwa ambapo alilazwa katika Hospitali ya Kairuki kwa kilichodaiwa hakuwa na ushirikiano kati yake na wasanii wenzie.
Akikanusha taarifa hizo pamoja na kutomchangia fedha, Steve alisema:

Msanii wa filamu Bongo, Coletha Raymond ‘Koleta’.
“Tukianza kusema kila anayeumwa tuwe tunamchangia wanachama watakimbia na mfuko tuliokuwa nao utaisha na tutashindwa kufikia malengo, lakini sikupata taarifa za ugonjwa kuhusu Koleta na hata ningezipata asingeachwa,” alisema Steve huku Koleta akisisitiza kuwa anatengwa.
“Sijui kuna nini kinaendelea kwa upande wangu na sifahamu kwa nini sipewi taarifa kwa wakati na uongozi wangu kama ilivyo kwa wasanii wengine wa Bongo Movie, najisikia vibaya sana,” alisema Koleta.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger