UPDATE: MSIKILIZE 'M TO THE P' AKIZUNGUMZIA HALI YAKE YA SASA AKIWA HOSPITALINI SOUTH AFRICA...!!

Picha ya msanii M2 The P akitabasamu kwenye kitanda chake hospitalini, na kuonekana hali yake inaendelea vizuri



Sikiliza mahojiano kati ya mtangazaji Millard Ayo akiongea na M2 The P iliyofanyika hospitali alikolazwa msanii huyo. Msanii huyo alikutwa mahututi pamoja na msanii mwenzake, Albert “Ngwair” Mangwea, aliyefariki dunia wikiendi iliyopita. To the P anasema hali yake sasa inaendelea vizuri. Click play button hapa chini kusikiliza mahojiano hayo
Read more >>

HII NDIO HALI YA SASA YA MSANII M2P AKIWA HOSPITALINI BAABA YA KUZUSHIWA KIFO...!!

Msanii M To The P aliyepelekwa hospitali pamoja na marehemu Albert Mangwea, kwa sasa anaendelea vizuri na matibabu kama anavyoonekana kwenye picha katika hospitali ya Helen Joseph huko nchini Afrika ya Kusini. (Picha kwa hisani ya Clouds FM)
Read more >>

KIJANA ANUSURIKA KUFA BAADA YA VIBAKA KUMCHOMA MOTO HUKO LINDI


Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Ismai Mayoba(31) anayefanya kazi Bar ya Mangrove,Mkazi wa Manispaa ya Lindi amenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kundi la Vijana waliotaka kumpora na hatimae kumchoma moto. 

Kwa sasa kijana huyo amelazwa katika Hospital ya Sokoine Mjini humo.

Kufuatia tukio hilo,Jeshi la Polisi wilayani Lindi limefanikiwa kumkamata mtu  mmoja kati ya watuhumiwa saba waliohusika na tukio hilo lilitokea katika eneo la Mtaa wa Congo.


Akithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kukamatwa kwa mtuhumiwa,Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi,Renatha Mzinga alimtaja ndugu Ally Manially(22)mkazi wa mtaa wa Kongo kuwa anashikiliwa na Jeshi hilo na atafikishwa mahakamani leo kujibu shitaka la kujeruhi na kujipatia pesa kwa njia ya Udanganyifu ikiwa pamoja na kumchoma mwenzie Moto huku akijua ni kosa kisheria.

Aidha Mzinga alieleza kuwa Jeshi la polisi linaendelea kutafuta watuhumiwa wengine 6 waliohusika na tukio hilo
Read more >>

VIDEO: HUU NDO UCHAFU UNAOTENDEKA NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA.

Hii ni video inayoonesha  uchafu  unaotendeka  ndani ya jumba la Big Brother Africa....
 
Nashindwa  kuusimulia, ila jionee mwenywe  katika  video  hiyo.....
Read more >>

ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU NDOA ZA JINSIA MOJA.....ADHABU YAKE NI KIFUNGO CHA MAISHA JELA..!!

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imetunga sheria ya kupiga marufuku ndoa za watu wa jinsia moja.Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Bwana Abubakar Khamis Bakar, aliyasema hayo kwenye Kikao cha Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi, Saleh Nassor Juma kutoka Chama cha Wananchi (CUF).

Katika swali lake, Bw. Saleh Nassor Juma alitaka kujua ni lini Serikali ya Zanzibar itatunga sheria ya kukataza ndoa hizo na kuweka adhabu kali kwa watu ambao watabainika kufanya vitendo hivyo vichafu. 


Waziri Abubakar amesema, ndoa za watu wa jinsia moja ni kinyume na utamaduni wa Zanzibar na kwamba sheria hiyo imeweka adhabu ya kifungo cha miaka saba kwa wale wote watakaopatikana na hatia hiyo.

Pia alisema kama ninavyomnukuu: "Sheria hii inahusu makosa mengi yakiwemo ya ubakaji, zinaa, usagaji na umalaya ambayo yote yana adhabu ya kifungo cha maisha au miaka isiyopungua 30 gerezani," mwisho wa kunukuu.
Read more >>

MZUMBE SECONDARY YAFUNGWA...WANAFUNZI WAPEWA SIKU 2 KUONDOKA KATIKA MAENEO YA SHULE..!!

Wananfunzi wakidato cha kwanza hadi cha sita katika shule ya sekondari Mzumbe Morogoro wamelazimika kuandamana kwenda ofisi ya mkuu wa mkoa wa huo wakishinikiza kuboreshewa huduma muhimu.

Maboresha wanayodai kuboreshewa shuleni hapo ni pamoja na miundombinu, kuondoa ubadhirifu, uongozi mbovu na kukomeshwa vitendo vya lugha chafu zinazo tolewa na baadhi ya walimu.

Maandamano hayo yalizimwa mapema asubuhi baada ya jeshi la polisi kulazimika kufika katika eneo la
sangasanga barabara kuu ya Iringa Morogoro ambapo maandamano hayo yalikuwa yamefika kuelekea katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro.

Wananfunzi hawa wa shule ya sekondari Mzumbe Morogoro ya wenye vipaji maalum wanadai kuwa maandamano hayo yanatokea baada ya kuvumilia kwa muda mrefu na hivyo wameamua kupaza sauti zao wakibainisha matatizo lukuki yanayo wasibu ambayo yanaweza kushusha kiwango cha taaluma yao.

Mkuu wa shule ya sekondari Mzumbe Dismas Njawa ameelezea namna alivyoweza kutatua baadhi ya matatizo lakini hayakukidhi haja za wanafunzi hao.

Katibu tawala Mkoa wa Morogoro Elia Ntandu alilazimika kwenda kuzungumza na wanafunzi hao akiahidi kuyafanyia kazi yale yatakayo wezekana.



Wanafunzi hawakuelewa, na ndipo Serikali ilipoamua kuifunga shule ya Sekondari ya vipaji maalumu, Mzumbe kwa muda usiofahamika na kuwapa wanafunzi siku mbili, kuanzia leo, kuondoka shuleni hapo
---
Monica Lyampawe,
TBC Morogoro.
Read more >>

HII NDIO TASWIRA YA MAANDALIZI YA MAZISHI YA MAREHEMU ALBERT MANGWEA HUKO MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM..!



 

 
 
 
 
 

MAOMBOLEZO ya msiba wa aliyekuwa mwanamuziki wa kizazi kipya, marehemu Albert Mangwea, yameanza  nyumbanmi kwa baba yake mdogo, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam ambako jana jioni ndugu, jamaa na majirani walikutwa wakiwa katika matayarisho ya kuupokea mwili wa marehemu.
Read more >>

AJALI: AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIA KICHWA WAKATI AKIPANDA DALA DALA MAENEO YA ILALA BOMA...!!

afariki-akidandia-daladala-0
afariki-akidandia-daladala
Mtu mmoja ambaye jina lake bado halijafahamika, amefariki dunia baada ya kuteleza na kuanguka wakati alipokua akijaribu kudandia Daladala maeneo ya Ilala Boma, Jijini Dar es Salaam, asubuhi leo. Marehemu huyo baada ya kuanguka na kupiga kichwa kwenye lami, alipasuka kichwa na kuvuja damu nyingi kichwani, na kufariki katika eneo la tukio.
Read more >>

VIDEO YA WASICHANA WALIONASWA WAKISAGANA DAR.....NI LAANA TUPU..!!


Maadili ya kitanzania yamekuwa yakiporomoka kila kukicha.Hili  limejidhihirisha  tena  baada  ya  kundi  la  akina  dada  kunaswa likiwa  katika  mchakato  wa  kusagana.....



Kundi  hili  linaloongozwa  na  mdada  aliyefahamika  kwa  jina moja  la Aziza, lilikuwa  katika  chumba   ambacho  wadada  hao  walikuwa  wakicheza  uchi  huku  wakisifiana  kuwa  ni  watamu ( baada  ya  kusagana)....



Haijafahamika  mara  moja  kama  wasichana  hao  ni  wanafunzi  au  siyo  wanafunzi....



Ndani ya video hiyo, wadada  hao  wanaonekana  wakifanya  uchafu  wao  huku  wakijirekodi   wenyewe.....



HII  NI  SEHEMU  FUPI  YA  VIDEO  HIYO..
video
Read more >>

KIFO CHA NGWEA BADO NI UTATA....PICHA YAKE AKIWA MOCHWARI IMEIBUA MASWALI MENGI YANAYOHITAJI UCHUNGUZI WA KINA.

KIFO cha msanii wa Hip Hop Bongo, Albert Kenneth Mangwea a.k.a Ngwea au Mangwair kilichotokea Jumanne wiki hii jijini Johannesburg, Afrika Kusini ‘Sauzi’, kimeendelea kuwagawa Watanzania katika makundi na kusababisha utata, Ijumaa linakuhabarisha

Kwa mujibu wa ripoti za awali za tukio hilo, Ngwea na mwenzake M 2 the P walizimika wakiwa usingizi ambapo wote walikimbizwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya St. Helen Joseph nchini humo.
Ilidaiwa kuwa katika harakati hizo ilithibitika kwamba Ngwea alishafariki dunia huku mwenzake akiwa hoi bin taaban.
Hata hivyo, hospitali hiyo haikueleza chanzo cha kifo hicho kwa sababu ya kusubiri uchunguzi wa mwili wa marehemu.
Habari za kifo cha msanii huyo zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii huku kila mtu akisema lake juu ya tukio hilo baya kwenye ulimwengu wa mastaa Bongo.
Ilisemekana kuwa kabla ya kukutwa na mauti, staa huyo wa ngoma ya Mkasi alikuwa nchini humo kwa ziara za kimuziki ambapo Jumanne iliyopita ndiyo ilikuwa arejee Bongo.


MADAI MAZITO KUTOKA SAUZI
Katika tukio hilo lililowagawa Watanzania, baadhi ya watu walidai kuwa inawezekana staa huyo aliuawa ili adhulumiwe mzigo wa ‘unga’ na watu waliokuwa wamempa tenda ya kuufikisha nchini humo huku wengine wakisema walijiovadozi na pombe kali.
“Katika hali ya kawaida inawezekanaje watu wawili wakajiovadozi kwa wakati mmoja? Kama ni ulevi, huo ni ulevi wa aina gani? Haiwezekani watu walewe sawa kisha wazimike sawa.
“Hapa kuna dalili ya kuwepo kwa  mchezo mchafu. Kifo cha Ngwea kina harufu ya kudhulumiana kwenye mzigo, si unajua siku hizi ndizo dili za baadhi ya wasanii wetu?” alidai Baba P kwenye mtandao wa Twitter.

ALIJIDUNGA MADAWA YA KULEVYA?
Madai mengine mazito ni kwamba eti wawili hao walijidunga madawa ya kulevya ambayo inasemekana yalikuwa feki au famba kama wanavyosema watu wanaodili na unga.
Kuhusu hilo ilidaiwa kuwa huenda unga waliokutana nao siku hiyo ulikuwa ‘kitu orijino’ tofauti na ule wa Kinondoni, Dar hivyo dozi iliwazidi.
Iliendelea kusemekana kuwa ukijiovadozi ‘kitu cha Sauzi’ huwa mtumiaji anagonga ‘kick’ kama wanavyosema watumiaji ambapo kitaalam huweza kusababisha kusimama ghafla kwa mapigo ya moyo kisha kifo.

KUZIDISHA BANGI?
Wapo waliodai kuwa huenda jamaa hao walizidisha matumizi ya kilevi cha bangi ambapo mjadala ulikuwa mkubwa, wengi wakihoji kama kuna uwezekano wa kilevi hicho kusababisha kifo.
“Nijuavyo mimi mtu akivuta bangi sana huweza kupata madhara katika ubongo lakini siamini kama inaweza kuua,” alisema Juma Kisaki akichangia juu ya kifo hicho mtandaoni.

ALILALA, ASUBUHI HAKUAMKA
Kwa mujibu wa watu waliokuwa na Ngwea katika nyumba aliyofikia kwa rafiki yake, jamaa huyo alilala vizuri lakini cha ajabu asubuhi hakuamka kama walivyopanga kwani alikuwa asafiri siku hiyo kurudi Bongo.
“Inawezekanaje mtu alale bila tatizo halafu afe usingizini? Kwa vyovyote kuna kitu. Au labda walipuliziwa sumu chumbani? Kwani hakukuwa na watu wengine ambao waliamka salama? Kweli ni utata juu ya utata,” aliandika Anonymous kwenye mtandao wa Twitter.

KWA NINI UTATA?
Ni utata kwa sababu hakuna uhakika wa moja kwa moja kwamba nini kilichukua uhai wa msanii huyo maarufu Bongo matokeo yake kila mtu anasema lake.

MAMA MANGWEA ANASEMAJE?
Akizungumza na ripota wa Ijumaa mjini Morogoro, Dustan Shekidele, mama mzazi wa Ngwea, Denisia Mangwea (63), alisema kitendo cha mwanaye huyo kumuahidi kwenda Morogoro kulifanyia ukarabati kaburi la marehemu baba yake kitabaki kichwani mwake kwa muda mrefu.
Akiwa nyumbani kwake Kihonda, Mazimbu Road, mama huyo alisema siku za karibuni aliongea na mwanaye kwa njia ya simu na kumuahidi kwenda Moro kulifanyia ukarabati kaburi la baba yake, marehemu Kenneth Mangwea.
”Albert aliniambia angekuja Morogoro wiki ijayo baada ya kutoka Afrika Kusini, leo (Jumatano) naambiwa naletewa maiti ambayo tutaizika jirani na kaburi la baba yake?” alihoji na kuangua kilio.
Mama huyo alisema kuwa Ngwea ni mwanaye wa sita na wa mwisho aliyemzaa mwaka 1982 ambaye hajawahi kumwambia kama ana mchumba au mtoto.

HALI YA DAR
Tofauti na Morogoro ambako watu walikuwa wamekusanyika nyumbani kwa wazazi wa marehemu, jijini Dar baadhi ya waombolezaji walionekana kuhangaika kutafuta sehemu ulipowekwa msiba wa msanii huyo.
Watu wengi walifika nyumbani kwa marehemu Sinza-Mori na wengine kwenda kwa kaka yake, Mbezi.
Hata hivyo, ilibainika kuwa kabla ya mwili wa marehemu kupelekwa Morogoro, utafikishwa Mbezi kwa kaka yake kisha kuelekea Morogoro kwa mazishi.
Wakati hayo yakiendelea, baadhi ya wasanii wa kada mbalimbali walikusanyika kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni, Dar kujipanga namna ya kuchangia chochote katika msiba huo wakati wakisubiri mwili uwasili kutoka Sauzi.

HALI YA MWILI WA MAREHEMU
Ijumaa lilifanikiwa kupata picha ya mwili wa marehemu. Kwa kuutazama tu alitokwa na damu puani na masikioni wakati akikata roho.

POMBE KALI ZAKUTWA CHUMBANI
Ilidaiwa kuwa ndani ya chumba alicholala Ngwea kulikuta bapa (chupa) mbili za pombe kali aina ya Vodka hali iliyowafanya baadhi ya watu kuamini pombe zilichangia kusindikiza kifo hicho.

RIPOTI FEKI YASAMBAA MTANDAONI
Katika hali ya kushangaza, juzi baadhi ya mitandao iliweka ripoti inayodaiwa ni feki.
Katika ripoti hiyo, ‘madaktari’ waliouchunguza mwili wa Ngwea walibaini kwamba kabla ya kifo chake yeye na mwenzake walizidisha kileo na unga.
Pia wawili hao eti hawakuwa na mpangilio mzuri wa chakula kwa maana kwamba walikuwa wakinywa pombe kali bila kupata msosi wa nguvu kama ‘nyama choma’.
Read more >>

MABINTI WACHAPANA MAKONDE WAKIGOMBEA MABWANA..!!

 Warembo wawili, wakazi wa Sinza, Dar es Salaam ambao majina yao hayakupatikana, wamenaswa wakizichapa laivu wakidaiwa kugombea bwana.

Tukio hilo la kujidhalilisha lilijiri katika baa maarufu ya Corner iliyopo Sinza-Afrikasana, Dar, majira ya asubuhi wakati watu wakiwa kwenye mishemishe za kuwahi kazini.
 

Katika tukio hilo, mmoja wa warembo hao alikuwa akilalamika kuwa kuna mwanaume walikubaliana kwenda kuvunja amri ya sita fastafasta ili awahi kazini lakini akazidiwa ujanja na shosti wake hivyo akataka kukomboa chake na ndipo alipotolewa manundu.

Habari kutoka eneo la tukio zilieleza kuwa warembo hao walijikuta wakizichapa kavukavu wakimgombea mwanaume huyo aliyedaiwa kuwa ni mume wa mtu, mwenye ndoa changa.
 
Katika timbwili hilo lililojaza kadamnasi, wanaume walishuhudia sinema ya bure baada ya mmoja wa warembo hao kula kipigo kizito na kuvuliwa nguo ambapo alibaki wazi sehemu za makalio.
Read more >>

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA YAKO HEWANI....YAANGALIE HAPA.


Matokeo  ya  kidato cha sita nayo yapo hewani.....Ukitaka  kuyaangalia  bofya  link  zifuatazo
au
Read more >>

TAARIFA MAALUM KUHUSU KUTEKWA NA KUUMIZWA KWA ABSALOM KIBANDA..!!

UTANGULIZI:Usiku wa Jumanne ya Machi 5 kuamkia Machi 6, 2013, Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, ambaye pia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda alivamiwa na kujeruhiwa vibaya akiwa nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake Mbezi Juu, Dar es Salaam.
Tukio hilo liliishtua na kutikisa taifa kwa kiwango kikubwa si tu katika tasnia ya habari nchini, bali pia jamii kwa ujumla hasa baada ya aina ya utekaji, utesaji na usiri uliotumika katika kufanikisha uhalifu huu kufanana kwa karibu na tukio lilomkuta Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madkatari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka lililotokea karibu miezi tisa kabla ya tukio la Kibanda yaani, usiku wa Juni 26, 2012.
Ukiacha matukio hayo, miezi sita kabla ya Kibanda kutekwa na kuteswa Mwandishi Daudi Mwangosi, aliuawa akiwa mikononi mwa vyombo vya dola Septemba 2, 2012 huko Nyololo, Iringa akiwa kazini.Tukio la Kibanda limekuwa na sura ya mwendelezo wa mauaji au utesaji wa wanahabari, hasa ikitiliwa maanani kuwa Mwandishi Issa Ngumba (45) wa Radio Kwizera aliyekuwa anafanyia kazi zake katika Wilaya ya Kakonko, Kigoma, Januari mwaka huu, alipigwa risasi na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha.Kama hiyo haitoshi, tukio la kutekwa na kudhuriwa kwa Kibanda limetokea mwezi mmoja tu baada ya Mwandishi wa Gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu kupigwa risasi na polisi akiwa nyumbani kwake Dar es Salaam kwa maelezo kuwa kimakosa polisi walidhani Matutu ni jambazi.Mazingira ya kutekwa na kuumizwa kwa Kibanda yalitia wasiwasi kuwa upo uwezekano, na dalili zilionyesha kwamba waliofanya kitendo hicho cha kinyama hawakuwa wezi wala majambazi kutokana na ukweli kwamba licha ya kuwa na fedha zipatazo shilingi milioni tatu taslimu ndani ya gari, laptop, simu tatu za gharama (ipad, iphone na Blackberry), watekaji hawa hawakuchukua chochote baada ya kukamilisha uhalifu wao.Kibanda aliumizwa kwa kiwango kikubwa. Alitobolewa jicho la kushoto, akaumizwa vibaya kichwani kiasi cha kusababisha kuvunjika kwa baadhi ya mifupa ya kichwa.

Aling’olewa meno mawili na kucha mbili, tena bila gazi. Watekaji hawa, katika unyama wa ajabu kabisa, walimkata pingiri ya kidole cha pete chini ya kucha na kuondokana nayo.Hali hiyo iliibua maswali mengi, watu wengi wakajiuliza na kutafuta sababu za kutekwa na kuumizwa kwa Kibanda kiasi hiki. Kutokana na kuwapo kwa maelezo mengi yanayotofautiana kuhusu tukio hilo, ikabidi Jukwaa la Wahariri Tanzania lifanye uamuzi.Katika kikao cha Machi 8, 2013 Jukwaa la Wahariri Tanzania liliunda TIMU ya watu watano na kuipa hadidu rejea za kufanya uchunguzi wa kihabari juu ya shambulio hilo kubaini limetokana na nini.

Timu hiyo iliundwa kufuatia uamuzi wa Jukwaa la Wahariri kufanya uchunguzi huo na baada ya kukubalika kwa ombi la ruzuku ya kufanya uchunguzi huo wa kihabari kutoka Mfuko wa Vyombo Vya Habari Tanzania (TMF). Ruzuku ya TMF ililenga kiujumla kutumia tukio la Kibanda kuwa chanzo cha kutengeneza mazingira salama zaidi kwa waandishi na wahariri na kwamba kiwango cha matukio ya kuteswa, kupigwa na kuuawa kwa waandishi yanapungua kila mwaka. Timu hii imefanya kazi usiku na mchana kwa kwa zaidi ya mwezi. Timu imezungumza na wadau 26.

Kati ya hawa yumo Kibanda mwenyewe, mke wake, ndugu zake, wasaidizi wake, waajiri wake wa zamani na wa sasa, viongozi wa kisiasa na vyombo vya dola kutafuta ukweli wa jambo hili. Pia tumesoma matamko na habari zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na magazeti ya kati ya Machi 5, 2012 na Aprili 5, 2012 kwa nia ya kufanya ulinganishi wa taarifa tulizozipata kutokana na uchunguzi na habari zilizochapishwa baada ya kutekwa kwake.Vyombo vya dola akiwamo Waziri mwenye dhamana walikataa kuhojiwa wakisema kuna tume ya serikali inayofanya kazi hiyo na kwamba kuhojiwa kungeonyesha kutokuwa na imani na tume hiyo.

Leo tunawasilisha muhtasari wa ripoti hii. Ripoti kubwa pamoja na viambatanisho vyake, itachapishwa na kuwekwa katika kitabu kimoja. Utaratibu mwingine wa kuchapisha habari ambazo hazijachapishwa kuhusiana na tukio hili (untold stories) pia utaandaliwa kwa ushirikiano na Jukwaa la Wahariri kwa nia ya kuieleza jamii maajabu juu ya kadhia hii.Tulipewa Hadidu Rejea ziafuatazo:

HADIDU REJEA:1. Kuchunguza mazingira ya kabla na baada ya tukio la kushambuliwa kwake. Kabla ya kushambuliwa kwa maana ya kufahamu kama kulikuwa na viashiria vyovyote vinavyoelekea kuwapo kwa mipango ya mashambulizi dhidi yake.2. Kuchunguza mazingira ya tukio lenyewe kwa kujikitika katika mwenendo wake hasa siku nzima ya Jumanne Machi 5, 2013.3. Kuangalia mazingira ya kazi ndani ya Kampuni ya New Habari (2006), Ltd na nje ya kampuni hiyo kwa kumulika sababu za kuhama kwake kutoka Free Media mwishoni mwa mwaka jana na kuhamia New Habari.4. Kuchunguza jambo jingine lolote linaloweza kutoa mwanga wa sababu za kuvamiwa na kupigwa kwa Kibanda.5. Kuchunguza mazingira ya sasa ya kazi kwa wanahabari na kupendekeza hatua za kuchukua kutokana na kile kitakachobainika

YALIYOJIRI KATIKA UCHUNGUZI:1.0. Kuchunguza mazingira ya kabla na baada ya tukio la kushambuliwa kwake. Kabla ya kushambuliwa kwa maana ya kufahamu kama kulikuwa na viashiria vyovyote vinavyoelekea kuwapo kwa mipango ya mashambulizi dhidi yake.Timu ya uchunguzi ilitumia muda mwingi katika eneo hili, kubaini iwapo kulikuwapo viashiria, sababu au matukio ya wazi yenye mwelekeo wa kujitokeza kwa shambulio hili. Tuliangalia pia iwapo wapo watu au makundi yaliyokwishapata kuonyesha ishara kwa matendo au kwa kauli juu ya uwapo wa nia hii. Uchunguzi umebaini kuwa kuliwapo viashiria vingi, isipokuwa Kibanda au watu wake wa karibu hawakupata kufikiri kuwa huenda vingeweza kuleta madhara makubwa kiasi hiki kama ifuatayo:-

1.1. Wiki tatu kabla ya Kibanda kuvamiwa, kutekwa na kuumizwa, gari la polisi aina ya gofu Na PT 180 liliwafuatilia kwa muda mrefu Absalom Kibanda na Ofisa Mtendaji Mkuu wa New Habari (2006) Ltd, Hussein Bashe likiwa limeegeshwa nje ya ofisi zao Sinza Kijiweni na baadaye likawafuatilia hadi Sinza Makaburini, ambapo walisimamisha magari yao na kuzungumza na polisi hao waliosema walikuwa wanatilia shaka magari yao. Baada ya kuzungumza kwa muda polisi waliondoka.
1.2. Usiku wa Februari 25, mwaka huu majira ya saa 09:00 usiku, Kibanda walivamiwa na watu walioingia kwenye uzio wa nyumba yao wakavunja kioo cha gari analotumia, lakini kioo kilipovunjwa ‘alarm’ ilipiga kelele, Kibanda akatoka nje na watu hao wakakimbia.

1.3. Kutokana na uvamizi huo, Kibanda na wapangaji wengine katika nyumba zilizopo kwenye uzio mmoja, waliona hatari ya kuvamiwa hivyo wakaanza mazungumzo na kampuni ya Ulinzi ya Kiwango, iliyowataka kufunga kamera za usalama na kuweka walinzi watano. Hadi Kibanda anatekwa, walikuwa hawajahitimisha mazungumzo na kampuni hii ya Kiwango.

1.4. Kuna askari anayefanya kazi Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) miezi minane kabla alipata kumpa Kibanda taarifa za kinteligensia, kuwa kulikuwapo mpango wa kumteka na kumuumiza. Taarifa kama hizo pia alipewa na wasamaria wanaofanya kazi katika Jeshi la Polisi. Kwa maneno yake Kibanda alisema:“Kuna rafiki yangu askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kama miezi minane au tisa hivi aliwahi kuniambia ‘unaandika sana usidhani kama watu wanakupenda. Chukua tahadhari hasa unapofika getini nyumbani kwako’. Tangu wakati huo nimekuwa nikichukua tahadhari sana.“Wiki mbili kabla ya tukio, niliwahi kuhisi kitu kama hicho [cha kuvamiwa] nikiwa getini. Nilipiga honi wakachelewa kuja kunifungulia, niliogopa sana. Hata nilipoingia ndani nilikuwa nimekosa raha kabisa.“Pia kuna rafiki zangu polisi waliwahi kuniambia kwamba ninatafutwa na kwamba watu wananifuatilia na ikibidi wanitengenezee ajali au kunifanyia kama Ulimboka au Kubenea.”

1.5. Ndani ya miezi mitatu mbele ya mlango wa ofisi yake Kibanda (Free Media Limited) ilikuwa mara kwa mara muda wa asubuhi anapofika ofisini anakuta damu. Haikufahamika kama damu hiyo ilikuwa ni ya binadamu, kuku, ng’ombe, kunguru au mbuzi, bali waliipuuza wakidhani ni masuala ya ushirikina. Mhariri Mtendaji wa sasa, Ansbert Ngurumo, amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo.1.6. Mfanyakazi mwandamizi wa Kampuni ya New Habari anakofanya kazi sasa Kibanda ndani ya wiki mbili kabla ya kutekwa na kuumizwa kwake alipata kumwabia Kibanda maneno mazito mara tatu, na hapa tunamnukuhu Kibanda:“Aliniambia Danny Mwakiteleko [aliyekuwa Naibu Mhariri Mtendaji wa New Habari] hakufa kwa ajali, bali alikufa kutokana na blood clotting (kuganda kwa damu). Hivyo ikitokea mtu ukapata ajali au ukapigwa na kuumizwa sana sehemu za kichwa hivi au tumbo, ni lazima madaktari wadhibiti sana blood clotting.“Na kweli, nilivyoletwa hapa Milpark hospitalini, madaktari walikuwa wananidunga sindano sita kila siku kwenye kitovu kuzuia blood clotting. …. (jina linahifadhiwa) aliniambia maneno haya mara tatu, katika mazingira yasiliyotarajiwa na kwa msisitizo ambao sikujua maana yake. Nasema …. (jina linahifadhiwa) naye achunguzwe kwa kina. Inawezekana kuna jambo analijua.”Ofisa huyu, alipishana dakika chache na Kibanda muda wa kutoka ofisini baada ya kipindi cha kwanza cha mechi kati ya Real Madrid na Manchester united kumaliza nusu ya kwanza (half time). Dakika ishirini baadaye Kibanda alishambuliwa.

2.0. Kuchunguza mazingira ya tukio lenyewe kwa kujikitika katika mwenendo wake hasa siku nzima ya Jumanne Machi 5, 2013.2.1.Familia ya Kibanda na Kibanda Mwenyewe hawakuwa na wasiwasi wowote siku hiyo kwani hawakuwa na hisia wala wazo kuwa ungetokea uvamizi huo.

2.2. Kibanda alipopiga honi, mlinzi alisogea langoni kumfungulia. Ghafla akasikia kishindo kikubwa. Akasikia kelele za Kibanda akiomba msaada. Kijana huyu Baraka Ibrahim mwenye umri wa miaka 27, aliogopa. Aliogopa kwa mana hakuwa na silaha yoyote mkononi. Hakuwa na panga, kisu, rungu, wala filimbi. Kwa maneno yake anasema:“Nilivyoona ningefungua geti hata mimi ningekufa, nilikimbia kuwaamsha majirani. Sikuwa hata na namba ya simu ya mtu yeyote kati ya mabosi wangu ninaowalinda. Nilikuwa mimi tu, imani yangu na Mungu wangu…. kutokana na maisha naifanya hivyo hivyo tu. Vinginevyo milele nisingefanya kazi hii ya ulinzi.”Mlinzi huyo alikimbilia kwa majirani katika nyumba aliyoamini yumo mwanaume, lakini akaanza kumwamsha House Girl, ili house girl amwamshe baba mwenyenyumba. Kitendo cha kuamshana na kuwapa taarifa kilichukua dakika tano hadi saba, na ndani ya muda huo, Mlinzi anasema watekaji wa Kibanda walifanyafanya unyama na uasi huo na kuondoka ndani ya muda mfupi kiasi hicho. “Watu hawa wana mafunzo maalumu,” anahitimisha.

2.3. Mke wake alikwenda kazini asubuhi na kurejea nyumbani jioni, lakini tofauti na utaratibu wake wa kawaida ambapo huwa anaangalia televisheni sebuleni hadi Kibanda anaporejea nyumbani, siku hiyo alikwenda kuangalia televisheni akiwa chumbani na usingizi ukampitia. Anasema hakusikia honi wala tukio la Kibanda kutekwa. “Hii inanitesa sana moyoni. Najiuliza kwa nini siku hiyo tu sikukaa sebuleni? Kwa nini siku hiyo tu nimelala mapema kabla Baba Joshua hajarudi (machozi yanamlengalenga). Najiuliza sipati jibu.”2.4. Mmoja kati ya wasaidizi wawili wa nyumbani kwa Kibanda, alisikia kelele za Kibanda akiomba msaada. Alimwamsha mwenzake na kumwambia. “Nasikia Baba Joshua anapiga kelele kama amevamiwa hivi.” Mwenzake alimwambia “Unaota maana kuna kelele za mpira.” Siku hiyo kulikuwa na mechi kati ya Real Madrid na Manchester United.Ni kweli zilikuwapo pia kelele za wanaoshangilia mpira siku hiyo, hivyo Kibanda alipoomba msaada, hata waliosikia walidhani watu wanashangilia mpira. Binti aliwaamsha Angela na mwenzake, wakaenda sebuleni, wakakaa na kuchungulia dirishani, wakaona mwanga wa gari getini, lakini baada ya kutosikia kelele yoyote wakarejea kulala wakidhani siye. Lakini binti mmoja alibaki sebuleni. Baada ya muda jirani mmoja akampigia simu Angela kumweleza kuwa mumewe ameshambuliwa.2.5. Kibanda kwa upande wake, anasema alipofika getini, alipiga honi, ghafla akaona watu wawili wamesimama pembeni mwa gari lake na mtu wa tatu akiwa kwa mbali. Kisha akasikia kishindo kikubwa, akidhani wanataka kuiba gari, aliatokea mlango wa abiria na kuanza kukimbia huku akiita. “Mama Joshua nisaidieeeeee.”Katika kukimbia, aliteleza akaanguka. Huku watesaji wake wakisema mara tatu “Afande piga risasi.” Kibanda alijaribu kupambana, akashika rungu, akawahoji amewakosea nini hadi wampige kiasi hicho, lakini hawakumjibu lolote. Waliendelea kumpiga, hadi akapoteza fahamu. Hakujua jicho limetobolewa saa ngapi, meno yameng’olewaje na wala pingiri ya kidole chake imekatawaje. Ifuatayo ni sauti ya Kibanda mwenyewe. Inasikitisha ila tuwe wavumilivu na tuisikilize.

3.0. Kuangalia mazingira ya kazi ndani ya Kampuni ya New Habari (2006) Ltd na nje ya kampuni hiyo kwa kumulika sababu za kuhama kwake kutoka Free Media mwishoni mwa mwaka jana na kuhamia New Habari.

3.1. Mazingira ya kazi ndani ya New Habari (2006) Limited na Freemedia Limited, yanaacha maswali kadhaa yenye kustahili majibu. Kama ilivyoelezwa kwenye Hadidu Rejea Na: 1, ndani ya kampuni ya New Habari imekuwapo misuguano isiyo na afya kwa kazi ya Kibanda kama mwandishi na tasnia ya habari kwa ujumla.

3.2.Mazingira ya kazi ndani ya Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ni utata. Uhusiano katika chumba cha habari si mzuri. Ndani ya kampuni hawaaminiani na imefikia hatua wanatuhumiana kuwa huenda baadhi ya viongozi ndani ya New Habari wamehusika kumteka na kumuumiza Kibanda. Haya yameandikwa ndani ya mitandao ya kijamii, ikidai kwamba kiongozi mmoja ndani ya kampuni hiyo alihusika na utekaji wa Kibanda.Mkurugenzi wa Uhariri, Prince Bagenda anasema waliohusika kusambaza taarifa chafu dhidi ya kiongozi huyo wa New Habari wanatoka ndani ya kampuni hiyo.

3.3. Timu ya uchunguzi ilibaini kuwapo mgawanyiko mkubwa ndani ya New Habari (2006) Ltd kwa kuwapo kundi la ‘Habari Wazawa’ na ‘Habari wa Kuja’. Malalamiko mengi yanajikita katika msingi kuwa ajira hazitangazwi na watu wanaajiriwa bila kuzingatia sifa za kitaaluma.

3.4. Kibanda hakuhama Free Media kwa amani. Uchunguzi unaonyesha kuwa miezi kadhaa kabla ya kuondoka kwake alianza kupoteza mamlaka. Mwenyekiti wa Kampuni ya Free Media Ltd, Freeman Mbowe alianza kumsikiliza zaidi msaidizi wake ambaye alikuwa Naibu Mhariri Mtendaji, Ansbert Ngurumo kuliko yeye Kibanda. Kwa maneno yake, anasema:“Nilihofu kuwa Mbowe anaweza kutugombanisha. Nikaona ni bora niondoke nisije nikagombana na Mbowe au Ngurumo.”Anasema alianza kupoteza mamlaka yake na kutoaminika kwa mwajiri wake baada ya kuandika makala kuhusu Abdulrahman Kinana ambayo kabla ya kuiandika hakuwa na wazo la kuondoka. Yaliyofuata baada ya makala hiyo, yalimshukuma aondoke.

4.0. Kuchunguza jambo jingine lolote linaloweza kutoa mwanga wa sababu za kuvamiwa na kupigwa kwa Kibanda.

4.1. Uchunguzi ulifuatilia masuala mbalimbali ikiwamo miendendo ya watu waliotajwa kwa njia moja au nyingine kuhusinaa na tukio hili. Hata hivyo, karibu watu wote waliohojiwa, akiwamo Kibanda mwenyewe aliyeumizwa walimtaja kwa kutilia shaka mwenendo wa kijana Joseph Ludovick. Hofu yao, iliongezwa nguvu na maandishi aliyoyachapisha Ludovick kwenye mitandano ya kijamii siku ya Machi 6, 2013.

4.2. Usiku aliotekwa na kuumizwa Kibanda, Ludovick katika naye alidai kuwa ametekwa katika eneo la Shekilango na kupelekwa hadi Kigogo. Baada ya kutekwa aliibiwa kila kitu, ikiwamo begi, laptop, simu mbili, fedha taslimu Sh 35,000, akavuliwa nguo na kubaki na chupi tu. Pia alieleza kuwa alitoa taarifa hizo kituo cha polisi Mabibo.

4.3. Maelezo ya Ludovick yalitiliwa shaka na watu wengi hasa baada ya kuleeza kuwa watekaji walitumia muda wa saa mbili kumtoa Shekilango hadi Mabibo, umbali ambao kwa kiwaida mwendo wake hauwezi kuzidi dakika 10. 4.4. Daniel Chongolo aliiambia timu kuwa alfajiri ya Machi 6, siku anayodai kutekwa Ludovick yeye alimuona eneo la Mabibo wakati anatoka Muhimbili. Chongolo alikwenda kituo cha polisi Mabibo na kupewa taarifa kuwa Ludovick alitoa taarifa polisi kuwa alikuwa ametekwa ila akarudishiwa mali zake zote. “Alipouliza amefuata nini polisi, akawambia kama raia mwema amefika kuandikisha kumbukumbu kwa nia ya kuonyesha kiwango cha uhalifu kinavyoongezeka nchini,” anasema Chongolo. Timu ya uchunguzi ilikataliwa kupitia leja ya polisi kama itakavyoelezwa hapa chini.

4.5. Pia taarifa za uchunguzi wa timu hii zinathibitisha kuwapo kwa utata juu ya madai ya kuibwa kwa simu za Joseph Ludovick, kwani simu yake ya tigo (inayodaiwa kuibwa) ilitumika saa 01:21 asubuhi siku ya Machi 6, 2013. Muda huu ofisi za Serikali na Kampuni ya Tigo zilikuwa hazijafunguliwa

5.0. Kuchunguza mazingira ya sasa ya kazi kwa wanahabari na kupendekeza hatua za kuchukua kutokana na kile kitakachobainika.

5.1. Uchunguzi umebaini kuwa maisha ya wanahabari yapo hatarini. Hatari hii inatokana na makundi mengi yenye masilahi kuwaona wanahabari wanaosimamia ukweli kuwa maadui wa masilahi yao haramu. Kuna hatari kubwa inayowakabili waandishi wakati nchi inapoelekea kwenye uchaguzi wa mwaka 2015.

5.2. Uchunguzi umebaini kuwa usiri umepungua katika vyombo vya habari. Tofauti na zamani ambapo habari nyeti ziliandikwa kwa kuhifadhi majina ya waandishi wakitumia jina la MWANDISHI WETU. Simu hizi hata habari za kutisha waandishi wanaweka majina yao na hata wasipoweka, ndani ya vyumba vya habari vingi waandishi wapo tayari kutaja nani ameandika habari fulani.

5.3. Usaliti miongoni mwa waandishi wenyewe ndani ya vyumba vya habari unazidi kuongezeka na usipodhibitiwa hali itazidi kuwa mbaya zaidi. Mwenyekiti wa MOAT, Dk. Reginald Mengi anasema: “Hili ni jambo muhimu sana. Tuache usaliti vinginevyo wengi wataumia.”

5.4. Pia alishauri waandishi wa habari kurejea katika msingi wa taaluma, ambayo inawataka wao kuwa ndio wenye kuendesha vyombo vya habari badala ya kutegemea matakwa ya wamiliki au makundi yenye masilahi binafsi.

6.0. KILICHOBAINIKA:
6.1. Uchambuzi uliofanywa ni timu hii umebaini kuwa hoja nne zinazungumzwa kuhusiana na kutekwa na kuumizwa kwa Kibanda. Hoja hizi ni:-(i) Kazi yake ya uandishi wa habari(ii) Uhusiano wa kisiasa na vyama au wanasiasa mbalimbali(iii)Uhusiano wa kijamii ikiwamo mapenzi(iv) Vitendo vya rushwa.

6.2. Timu imejiridhisha kutokana na majibu ya wengi kuwa dhana ya mapenzi na rushwa, havina nafasi yoyote katika tukio hili. Wote waliohojiwa walieleza pasi na shaka kwamba suala hili la kushambuliwa na kuumizwa kwa kiwango kikubwa kwa Kibanda, halina uhusiano wowote na rushwa au mapenzi.

6.3. Kutokana na yaliyotajwa hapo juu kazi yake na siasa vikiunganishwa vimechangia kwa kiasi kikubwa kuvamiwa kwa Kibanda. Timu imebaini kuwa kuna kutupiana mpira kati ya vyombo vya dola na vyama vya siasa. Mchezo huu mchafu unaweza ukawa mwanzo wa kuumizwa kwa Kibanda na waandishin wengine.

6.4. Baadhi ya waliohojiwa walidai kuwa utekaji huu umefanywa na vyombo vya dola ukiwa sehemu ya mpango mkakati wa vyombo hivi kukihusisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na vitendo vya ugaidi.6.5. Wanayataja matukio ya Uchaguzi Mdogo wa Igunga, maandamano ya Morogoro na Mkanda anaodaiwa kurekodiwa Mkurugenzi wa Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare kuwa vililenga kukifanya CHADEMA kichukiwe na Watanzania kwa kukitaja kama chama cha kigaidi ambacho kinateka watu na kinawaumiza.

6.6. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe anadai kwamba mpango kama huo vyombo vya dola viliutumia kwa NCCR Mageuzi vikakisambaratisha, Chama cha Wananchi (CUF) kilisingiziwa udini kikapoteza mwelekeo na sasa vyombo hivyo vililenga kukifanya CHADEMA kionekane cha kigaidi mbele ya macho ya jamii ndiyo maana imerekodiwa mikanda kwa nia ya kuitumia kujenga hoja hiyo.

6.7. Wakati Mbowe akisema hayo, baadhi ya watu waliohojiwa wanadai kuwa CHADEMA kimepewa mafunzo na ushauri kutoka nje ya nchi kuwa kikitumia baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola wasiokuwa waaminifu kuteka, kuumiza na hata kuua baadhi ya watu maarufu nchini wakiwamo waandishi na wanasiasa, basi wananchi wataamini kuwa Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake kimeshindwa uongozi na sasa kimeanza kazi ya kuua wanaowapinga.

6.8. Kwa njia hiyo, inaelezwa kuwa hesabu za Chadema ni kuwa wananchi wataichukia CCM na Serikali yake na kukipa nafasi ya kuingia madarakani. Hapa kauli ya Chadema kuwa NCHI HAITATAWALIKA itakuwa imetimia.

6.9. Dhana nyingine iliyojitokeza ni kuwa wapo wafanyabiashara ambao wana vita binafsi, hivyo wanaamua kuumiza watu wasiowaunga mkono katika mipango yao na hilo ndilo limemkumba Kibanda, baada ya kuwa ameepusha mauaji ya mwandishi mmoja na aliyekuwa ameandaa mpango wa kuua mwandishi huyo hakuridhika hivyo akaamua amshughulikie Kibanda.

7.0. MAPENDEKEZO:Baada ya Timu kupata taarifa hizi na nyingine nyingi, inapendekeza yafuatayo:-

7.1. Taarifa hii ichukuliwe kama chanzo cha uchunguzi zaidi wa vyombo husika.7.2.

Yanahitajika marekebisho makubwa na ya haraka katika mifumo ya uendeshaji wa vyumba vya habari kwa nia ya kurejesha misingi ya uandishi wa habari inayokubalika.

7.3. Usalama wa wanahabari unapaswa kupewa kipaumbele na wamiliki, wanahabari wenyewe na jamii kwa ujumla. Hapa Timu inapendekeza yawepo mafunzo ya kuwawezesha wanahabari kutambua viashiria vya hatari na kuchukua hatua mara moja.

7.4. Kwa kiwango alichoumizwa Kibanda iwapo mwajiri wake asingejitolea kugharamia matibabu, hatujui hatima yake ingekuwaje leo hii. Tunapendekeza taasisi na mifuko mbalimbali inayojihusisha na masuala ya wanahabari kama Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) , Baraza la Habari Tanzania (MCT), Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kuanzisha mfuko wa pamoja utakaotumika kugharamia matibabu ya waandishi watakaoumia wakiwa kazini.

7.5. Tukio la kutekwa kwa Kibanda limeonyesha mwanga kuwa wahariri tumegawanyika mno. Habari zilizochapishwa katika magazeti mbalimbali na mitandao ya kijamii zimeonyesha haja ya kuwafanya wahariri kuwa kitu kimoja kwa kuondoa tofauti zao zisizo na masilahi kwa tasnia ya habari.

7.6. Kuna viashiria vingi kuwa kuelekea mwaka 2015 matukio ya waandishi kuumizwa au kutekwa yanaweza kuongezeka kutokana na wanasiasa na vyama kuwania madaraka huku wakitumia baadhi ya watumishi katika vyombo vya dola. Kwa mantiki hiyo, vyombo vya habari na waandishi wa habari wachukue tahadhari kuanzia sasa.

7.7. Taasisi za habari zifanye juhudi za makusudi kukutana na vyama viwili vya siasa vya CCM na CHADEMA haraka iwezekanavyo, kuzungumzia viashiria hivi vya hatari vinavyoelekea kuvuruga amani ya Tanzania.

8.0. HITIMISHO:Ni dhahiri kuwa kupigwa na kuteswa kwa Kibanda kumejiegemeza katika siasa na kazi yake, hali inayofanya makundi muhimu kuchukua wajibu wa msingi. Kwa upande wa Serikali ni muhimu kufuatilia viashiria katika taarifa hii kwa nia ya kupata ukweli zaidi na kuchukua hatua stahiki za kisheria dhidi ya wahusika.Na kwa upande wa vyombo vya habari na taasisi za kihabari zinapaswa kutambua viashiria vinavyohatarisha usalama wa waandishi wa habari na wahariri na kutengeneza mazingira yatayokuwa salama zaidi kwa waandishi kufanya kazi zao.

9.0. SHUKRANI:

9.1. Tunapenda kulishukuru Jukwaa la Wahariri Tanzania, kwa kufanya uamuzi sahihi wa kuwezesha kufanyika kwa uchunguzi huu ulioanza kuonyesha mwanga wa nini kilitokea.

9.2. Tunapenda kulishukuru Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwa kushiriki kikamilifu na kuiwezesha timu hii kwa Rasilimali Watu na Mali kufanikisha kazi hii.

9.3. Tunapenda kuwashukuru Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) kwa uwezeshaji wa ruzuku, uliofanikisha kufanya uchunguzi wa kihabari uliohusisha kwenda nchini Afrika Kusini kufanya mahojiano na Kibanda. Uwezeshaji huo pia unahusisha kutengeneza mwongozo kwa waandishi wenye lengo la kuwaepusha na hatari za kiusalama.

9.4. Tunawashukuru Kibanda, mkewe Angela, wanafamilia, ndugu na jamaa wa Kibanda na wanahabari wote waliohojiwa kwa ushirikiano mkubwa walioutoa kwa Timu hii.

9.5. Tunawashukuru wahariri wote kila mtu kwa nafasi yake, kutokana na ushauri wa mara kwa mara mliotupatia katika kufanikisha uchunguzi huu.

10.0. WAJUMBE WA TIMU:Timu hii iliundwa na wajumbe watano ambalo ni:1. Deodatus Balile – Mwenyekiti2. Pili Mtambalike – Mjumbe3. Jane Mihanji – Mjumbe4. Tumaini Mwailenge – Mjumbe5. Rashid Kejo – Katibu
Read more >>

UPDATE: MSANII M2P ANAENDELEA VIZURI NA MATIBABU, MWILI WA NGWEA KULETWA J'MOSI YA TAREHE 1,JUNE.

Msanii M2 the P anaendelea vizuri, leo ameweza kuongea na ametolewa ICU kupelekwa wodini
-Mwili wa Albert Kenneth Mangwair unatarajiwa kuwasili jijini Dar Jumamosi Juni 1, 2013 na kuhifadhiwa katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili.
-Ngwair anatarajiwa kuagwa siku ya Jumapili katika Viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar.
-Msanii Bushoke alaani watu wanaotoa taarifa zisizo sahii kuhusu sababu za kifo cha Ngwair. Baadhi ya wasanii ambao wamefika kumuona msanii M to the P ni Bushoke ambaye yeye yuko Afrika ya Kusini kwa wazazi wake pamoja na watanzania wengine wanaoishi huko wamesema hali yake inaendelea vizuri. 

Rafiki wa karibu wa M to the P ambaye amesema yeye anaishi na M to the P na ni kama kaka yake kwani wanakaa nyumba moja, Bright Job amesema M to the P hatumii aina yoyote ya dawa za kulevya.. Bado watanzania wanataka kujua ni nini kilichotokea Afrika ya Kusinii kusababisha madhara makubwa kwa wasanii hao na habari masai.co nayo inatafuta chanzo cha madhara hayo..

#N.B kuna baadhi ya WaTz walioko south ndio wanaotuma taarifa zisizo za kweli REST IN PEACE#
Read more >>

HII NDIO TWEET YA KIMAPENZI KATI YA MREMBO K'LYNE NA MHESHIMIWA REGINALD MENGI....ADAI KUWA NDIYE BABA WA MAPACHA WAKE WAWILI...!!

KATIKA kile kilichoonekana kuwa mapenzi haya Umri wala Rika leo katika pita pita zangu nimekutana na Tweet ya Msanii K'lyne akimtakia Happy Birthday kipenzi cha Roho yake Mheshimiwa Reginald  Mengi.


Kumekuwepo na Minong'ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa bwana Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili. Happy Birthday Mmili wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali TOP in town kimwana Jackline Ntuyabaliwe(K'lyne)  mapenzi hayana macho siku zote.

Hii ndio Tweet ya K'lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI
Read more >>

ANGALIA VIDEO YA LIPUMBA AKIKIRI KUMSAIDIA RAIS KIKWETE WAKATI WA UCHAGUZI 2010..!!

LIPUMBA AIBUA JAMBO ZITO - AKIRI KUMNUSURU KIKWETE UCHAGUZI MKUU MWAKA 2010

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na “kumnusuru” Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.

Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa.

Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.

Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.


“Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi,” alisema.

Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.

Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema “wenzetu wameanza kujipanga” kuelekea 2015.

“Kwahiyo kama Waislamu tunataka kupata haki zetu, kama tunataka kuishi kama raia wa daraja la kwanza katika nchi yetu, lazima tujipange kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; na sisi tuanze kujipanga kwa sababu wenzetu wameanza kujipanga, vinginevyo tutaendelea kubaki maskini na raia wa daraja la nne katika nchi yetu wenyewe.

“Mwaka 2010 wakati mshindi wa uchaguzi wa rais alipotangazwa, mimi nilikwenda kwenye hafla ya kutangazwa matokeo, na nilikwenda makusudi tu, siyo kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, ila nilikwenda makusudi kwa kujua hali ya kisiasa ilivyokuwa wakati huo.

“Huku nilikutana na Sheikh Basaleh. Nilipokutana naye, alinipongeza; sijui kama yeye anakumbuka, akaniambia ‘umeweka mbele imani yako na umekuwa mwelewa wa mambo.’”

Hata hivyo, licha ya Profesa Lipumba kuwaambia Waislamu wajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu, hakusema wajipange kupitia chama kipi.

Lakini alisisitiza kwamba uchaguzi ujao ni zaidi ya siasa au rais yupi anafaa, bali maslahi, hasa ya rasilimali nyeti zinazopatikana katika ukanda wa Pwani ya Mashariki, eneo ambalo alisema linakaliwa zaidi na watu wenye imani ya Kiislamu.

Katika moja ya kauli zake, Profesa Lipumba alisema kwamba kuna chama kimoja kinataka kuchukua madaraka ya nchi, lakini kinasaidiwa na mataifa ya magharibi, yasiyoenzi wala kuthamini imani ya Kiislamu.

Kwa muda sasa, zimekuwapo tetesi kwamba CCM imekuwa inafanya siasa za udini dhidi ya vyama vya upinzani, hasa inapoona maslahi yake yapo hatarini.

Mwaka 2010 makada kadhaa wa CCM walitumia mitandao ya simu kuchonga (spoofing) ujumbe wa simu ulioshambulia mgombea mmoja wa upinzani, ukimhusisha na imani yake.

Kauli ya Lipumba imethibitisha pia minong’ono iliyokuwapo muda mrefu kuwa baadhi ya kura za Profesa Lipumba zilipotelea kwa Rais Kikwete.

Katika uchaguzi huo, Lipumba alitangazwa kushika namba ya tatu, nyuma ya Rais Kikwete na Dk. Willibrod Slaa wa CHADEMA.

Alipoulizwa kuhusu ziara yake msikitini na kauli aliyotoa, Profesa Lipumba alikiri kwamba alikwenda kuzungumzia hali ya kisiasa nchini.

Read more >>

TAARIFA YA MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE, UFAULU WAPANDA KWA ASILIMIA 23....YAANGALIE HAPA.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa.


Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza rasmi matokeo ya Kidato cha Nne 2012. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu.
Matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.
Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.
Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa yalionyesha kuwa kati ya watahiniwa 367,756 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana, waliokuwa wamefaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu walikuwa 126,847 sawa na asilimia 6.4. Waliopata daraja la nne walikuwa ni 103,327 sawa na asilimia 28.1.
Katika matokeo hayo, watahiniwa 240,909 sawa na asilimia 65.5 walipata sifuri, hesabu ambayo imebadilika katika matokeo mapya ambayo yanaonyesha kuwa sasa waliopata daraja hilo ni 158,100 ambayo ni asilimia 43.

KUPATA MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE 2012 >>BOFYA HAPA<<
Read more >>

HUU NDIO MWILI WA MAREHEMU MANGWEA UKIWA MONCHWARI....R.I.P MANGWEA..!!


BLOG HII INAOMBA RADHI KWA KUUONESHA MWILI WA MAREHEMU MANGWEA..
Read more >>

VIDEO YA AMMY NANDO WA TANZANIA NDANI YA BAFU MOJA NA MREMBO WA NAMIMBIA NDANI YA BBA....!!


Jana (May 29) ilikuwa ni usiku wa tatu katika jumba la big brother Afrika huko Afrika Kusini mengi yanazidi kuonekana na sasa washiriki wengi wanaanza kuonesha side B ya mioyo yao na kujaribu kupata muda wa kuwa romantic na kuonesha upendo (Romantic time).

 Wakati washiriki wengine wakiendelea na mambo yao mtanzania Ammy Nando alijiachia kwenye bafu moja na na kuoga na mrembo Dillish kutoka na Namibia ambae ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu akisomea Saikolojia.

Huenda huu ukawa mwanzo wa mahusiano yao humo ndani kwa sababu moyo hauna pazia na uzuri wa Dillish unaweza kumvuta to the limit model huyo wa kitanzania.

 Kwa upande mwingine the boss lady toka Kenya Huddah Monroe alipata nafasi ya kushare na  Denzel mawili matatu hasa kuhusu mahusiano, wakati Denzel akiwa ameonesha tangu mwanzo kudata kwa Huddah. 



Jana Huddah alifunguka na kumwambia kuwa anahitaji mwanamme mwenye pesa na kwamba she is a gold digger.
 

Wiki hii Benzel, Betty, Huddah, Selly na Natasha wako katika nafasi ya  kukumbwa na Eviction

VIDEO  YAO:


Read more >>

"CUF NI CHAMA CHA MASHOGA KINACHOUNGA MKONO NDOA ZA JINSIA MOJA NA USAGAJI"...WENJE

Wenje achafua bunge. asema CUF ni chama cha liberal kinachounga mkono ndoa ya jinsia moja, ushoga na usagaji! wabunge wa CUF waja juu na kumpromoshea matusi na kumtaka aondoe hayo maneno. yeye akaanza kutoa ufafanuzi lakini wabunge wote wa CUF wakasimama na kuanza kumfokea Wenje kwa maneno makali huku wakisisitiza kuwa bila kuondoa hayo hakisomwi kitu leo! Naibu Spika kasitisha bunge mpaka ...
Bunge lachafuka na kuahirishwa baada ya CUF kuhusishwa na usagaj na ndoa za jinsia moja


wakati akisoma hotuba ya kambi ya upinzan mh wenje alisema CUF wana urafik na chama cha Liberal ambacho kina msimamo kuruhusu ndoa za jinsia moja na usagaj.mbunge wa Cuf aliomba mwongozo na hatimaye vurugu kusikika na vipigo.
Read more >>

HIVI NDIVYO JINSI MAMA WA MSANII DUDE ALIVYOKATA ROHO MBELE YA MWANAYE....INASIKITISHA SANA..!!

INAUMA sana! Staa wa maigizo ya runingani na filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amepata pigo kubwa la mama yake mzazi aitwaye  Mwadodo Ramadhan maarufu kwa jina la ‘Bi. Dodo’ kukata roho mikononi mwake akiwa anamkimbiza hospitali kwa ajili ya kuokoa uhai wake.

Dude akiwa na mama yake kabla hajakata roho.
SEHEMU YA TUKIO
Kwa mujibu wa chanzo chetu, mama huyo aliaga dunia ghafla usiku wa kuamkia Jumanne wiki hii akiwa ametolewa nyumbani kwa mwigizaji huyo, Ilala-Bungoni na kukimbizwa Hospitali ya Amana, jijini Dar es Salaam.
“Dude alikuwa akiishi na mama yake mzazi licha ya kwamba hapa Dar ana ndugu wengine, mpaka mauti yanamkuta alikuwa akiishi nyumbani kwake na siku ya kifo alikuwa akimuwahisha hospitali ya Amana,” kilisema chanzo.

ALIJUA MAPEMA ATAKUFA, AFANYA MAAJABU
Kwa mujibu wa chanzo hicho, siku moja kabla ya kifo cha mama huyo, yaani Jumatatu, marehemu alitembea sana. Alisema marehemu alikwenda sehemu mbalimbali za Jiji la Dar wanazoishi watoto wake wengine kwa lengo la kuwajulia hali, jambo ambalo ni kama la ajabu kwani siku za nyuma hakuwa mtu wa kusema anawatembelea watoto wote kwa siku moja.
“Inashangaza sana na naweza kusema ni ajabu kwani siku ya Jumatatu mama alimuaga mwanaye Dude kwamba anakwenda kuwasalimia ndugu zake wengine na angerudi jioni ya siku hiyohiyo, Dude akamkubalia na akampa nauli, akamwambia akawasalimie aendako,” kilisema chanzo.
Kikaendelea: Naamini kiroho marehemu alijua kifo kinamuita, sasa alikwenda kuwaaga watoto wake kwa vile hawataonana tena. Unajua mambo ya Mungu ni mengi sana, unaweza ukawa hujui lini utaondoka lakini ukafanya mambo yenye kuashiria kutambua kifo.


...Dude akizidi kupigania uhai wa mama yake.
SIKU YA TUKIO
Kwa mujibu wa Dude, siku ya kifo cha mama yake, yaani Jumanne yeye hakuwepo nyumbani, alitoka kidogo, aliporudi alimkuta Bi. Dodo akiwa katika hali mbaya, jambo lililomshangaza sana.
“Mimi sikuwepo, niliporudi nikamkuta mama yupo katika hali mbaya sana wakati nilimwacha mzima kabisa, nikashangaa sana. Nilijaribu kumuuliza anaumwa nini, hakujibu kitu wala hakuonesha kuelewa chochote kile. Nilishtuka kidogo.
“Moyoni niliamini amepoteza fahamu tu kutokana na hali aliyokumbana nayo. Ilibidi tumkimbize Hospitali ya Amana ili madaktari wakampime na kugundua nini kilimsibu ghafla wakati alikuwa mzima wa afya. Mpaka hapo nilikuwa najipa moyo kwamba nakwenda na mama lakini nitarudi naye.”
Alisema pia aliwasiliana na ndugu mbalimbali wakiwemo wale waliotembelewa jana yake ili kuwajulisha kuhusu hali ya Bi. Dodo.

WAFIKA AMANA, MADAKTARI WANENA
Alisema walipofika Hospitali ya Amana, madaktari walimpima kwa vipimo vya kitaalam na kubaini kuwa mama Dude alishakata roho muda mfupi uliopita.
Walisema huenda mama huyo alikumbwa na mauti akiwa ndani ya gari kupelekwa hospitalini hapo ambapo Dude mwenyewe ndiye aliyemshika mama yake ndani ya gari hadi Amana.

KWA MUJIBU WA WATAALAM
Jumanne hiyohiyo, Amani lilizungumza na daktari mmoja (jina linahifadhiwa) wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhusu matatizo yanayowapata watu ghafla na kupoteza fahamu ambapo alisema:
“Mara nyingi ni mshtuko wa moyo, hasa nyakati za usiku. Hii huwapata watu wenye umri mkubwa kidogo au wale wenye msongo wa mawazo. Hali hii ikimpata mtu na akikata kauli hawezi kukaa sawa tena.”

KILIO CHA DUDE
“Sikujua kama nitampoteza mama yangu kwa siku hii (Jumanne) kwa sababu hakuwahi kunilalamikia kuhusu kuhisi maumivu yoyote yale,” alisema Dude.
Akaongeza: Naumia sana, siamini lakini najua imeshatokea, sina la kufanya, mama yangu hayupo tena duniani.
Alisema anamuombea mama yake afike salama safari yake hiyo kwani ameondoka ghafla na hakuwa akisumbuliwa na ugonjwa wowote, akaongeza ni mipango ya Mungu hivyo hawezi kumlaumu.
Marehemu Bi. Dodo alitarajiwa kuzikwa jana  (Jumatano), saa 10:00 kwenye Makaburi ya Ilala baada ya taratibu zote kufanyika.
Read more >>

OMBA OMBA FEKI ALIYEJIFANYA KUWA HANA MIKONO ALA KICHAPO KIKALI KUTOKA KWA WANANCHI HUKO IRINGA....SOMA MKASA HUO HAPA..!!

WAKAZI wa mjini Iringa hivi karibuni wameshuhudia kituko cha mwaka baada ya kumnasa mzee mmoja akijifanya ombaomba kwa kuigiza ulemavu asiokuwa nao.
...akipewa kichapo baada ya kubainika ana mikono yote miwili.

Ombaomba huyo feki alijifanya hana mkono wa kushoto na mguu wa kulia na kuweka pozi la kuomba kama vile ni mlemavu katika eneo la Hazina Ndogo, mjini hapa.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, mlemavu huyo feki ameumbuliwa na mtu mmoja ambaye alimuona asubuhi ya siku ya tukio akiwa hana ulemavu wowote kabla ya kumkuta mchana akiomba kwa kujifanya ni mlemavu wa mkono na mguu.
Mtu huyo aliwaambia baadhi ya wananchi siri ya ombaomba huyo na kuwafanya kupandwa na hasira na kuanza kumshushia kipigo wakitaka kuhakikisha kama kweli ni mzima kiasi cha kumuumiza usoni.


...Akitoka nduki baada ya kushtukiwa na wananchi.
Kwa hofu ya kuuawa, mlemavu huyo feki alijinusuru kwa kuonesha mkono wake wa kushoto aliokuwa ameuficha ndani ya koti alilolivaa na mguu aliokuwa ameukunja na kuukalia.
Wakati wananchi wenye hasira wakiendelea kumpiga, mzee huyo alijitahidi kupata upenyo na kutimua mbio ndefu kukimbilia eneo la Miyomboni na kuwaacha watu wengine wakiwa hawana mbavu kwa vicheko.



Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walipoongea na mwandishi wetu walisema wakati mwingine ombaomba huyo hujifanya bubu na kuwaomba watu fedha za matibabu.

 
Ombaomba feki akijifanya hana mkono.
 Inadaiwa kuwa hii si mara ya kwanza kwa ombaomba huyo kushtukiwa akifanya mchezo huo, awali alishawahi kufukuzwa katika Kitongoji cha Santoni mjini hapa.

...Akizidi kuchezea kichapo.
“Bahati yake amekimbia kama tukimkuta tena akijidai ni mlemavu tutamvunja mkono na mguu ili awe mlemavu kweli,” alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Tuhuma nyingine zinasema kuwa ombaomba huyo hutumia mbinu hizo za kitapeli kwa kuwa amekimbiwa na mpenzi kutokana na kutokuwa na kipato.
Wananchi hao wenye hasira wameutaka uongozi wa Manispaa ya Iringa kuwabana ombaomba wote wanatumia udanganyifu kujipatia fedha na kutaka kuwepo kwa utaratibu maalum wa kuwasaidia wanaohitaji misaada ya kweli.
Read more >>

VIDEO: MSIKILIZE P-FUNK AKITOKWA MACHOZI MSIBANI NA KUTOA ONYO KALI KWA 'CLOUDS FM' KUHUSU KUPIGA NYIMBO ZA MANGWEA...!!



 

Kinachoendelea hivi sasa katika viwanja vya Leaders Club sasa ni kuwa karibuni wasanii wote pamoja wakishirikiana na familia ya Marehemu Albert Mangwair wamekutana kwaajili ya kupanga mikakati ya mazishi pamoja na kukusanya Rambi Rambi kwaajili ya msiba huo.

Hizi ni baadhi ya picha ambazo zinaonyesha baadhi ya wasanii na watu mbalimbali wakiwa katika viwanja hivyo.

Mmoja wa Ndugu Zake Marehemu Ngwair.
Mmoja wa Ndugu Zake Marehemu Ngwair.

ngwea.....

ngwea.......

ngwea....

ngwea...

ngwea........



Wakati Huo Huo Producer mkongwe katika game hii ya muziki, P-Funk Majani nae ameonesha ni jinsi gani alivyoguswa na na tukio hili la kuondokewa na msanii ambaye alikuwa ni rafiki yake wa karibu sana marehemu Albert Mangwair …

Majani ni producer pekee ambaye alishiriki kwa kiasi kikubwa kwa kuweza kufanya rapper Ngwair kutambulika katika game ya muziki wa Bongo Flava

Akiongea na mwandishi wetu kutoka GongaMx.Com, Majani ameeleza utayari wake katika kushirikiana na familia ya marehemu Albert Mangwair mpaka rafiki yake huyo atapozikwa

Mcheki MAJANI akiwa anaongelea suala zima kuhusina na msiba huu na utayari wake katika kushiriki 

MSIKILIZE P-FUNK...
Read more >>

Producer Mswaki Aimba kama Ngwear Kumuenzi-Sikiliza Wimbo Huo Hapa...!!

Huu Wimbo Ameimba Producer wa mziki anayejulikana kwa jina la Mswaki Kutoka Studio ya Black Curtains....Ameimba kama Marehemu Ngwear Akiimba baada ya Kifo chake...Sikiliza Hapa chini: Big up Sana Mswaki
Read more >>

SOMA HAPA CHAT YA MWISHO KATI YA MAREHEMU MANGWEA NA WEMA SEPETU KABLA YA KIFO CHAKE...!!

Katika dondoo zetu leo hii tuliweza kupata moja ya chat za mwisho mwisho ya marehemu Albert Mangwea akiwa afrika ya kusini na mwanadada wa bongo movies Wema sepetu. Katika maongezi hayo Ngwea alikuwa anapanga Kumtumia mwadadada mwingine wa bongo movies Kajala Masanja kwenye video yake mpya aliyokuwa anajiandaa kuifanya. Maongezi yao yalikuwa hivi.
Mangwea : kuku bandani..
Mangwea : Nataka Kajala…
Mangwea : Sikiza nyimbo then utanipa idea..
Mangwea : Nataka tukipiga hela kwa bro…
Mangwea : Tulipe na hela ya ticket ya Jux aje toka China tumalize huku kusini
Mangwea : #hugs
Wema Sepetu : Upo api?
Mangwea: Me nipo Pretoria now momo…
(Angalia screen shot ya maongezi hayo pichani)
Dah, inasikitisha sana. Maisha ya Msanii huyu yaliyokatika mapema. Mungu ailaze roho marehemu mahali pema peponi.
Read more >>

PICHA ZA WASANII WALIPOKUTANA LEADERS CLUB KUJADILI MAZISHI YA ALBERT MANGWEA...!!

Wasanii wa Bongo wa kusanyika LIDARZ CLUB kwenye kikao cha wasanii kuhusu mazishi ya mpendwa wao ALBERT MANGWEAR
Read more >>
Pages (38)1234 »
 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger